LEARNING

Jinsi ya kusali Rozali ya Huruma ya Mungu

Jinsi ya kusali Rozali ya Huruma ya Mungu

Jinsi ya kusali Rozali ya Huruma ya Mungu -Tumia Rozari ya kawaida kusali Rozari ya Huruma ya Mungu kama ifuatavyo:

*Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu ….Amina*

*Anza kwa sala hii….*

Yesu, ulikufa, lakini chanzo cha uhai kilitoka kwa ajili ya watu, na bahari ya huruma ilifunguka kwa ajili ya ulimwengu mzima. Ee chemchemi ya Uhai, huruma ya Mungu isiyo na mwisho, ikafunika ulimwengu mzima na ukajimwaga mwenyewe juu yetu.

*BABA YETU.*

*SALAMU MARIA….X3*

*KANUNI YA IMANI.*

Kila penye punje kubwa (Badala ya Baba yetu):

Baba wa Milele, ninakutolea Mwili na Damu, Roho na Umungu, wa Mwanao Mpenzi sana, Bwana wetu Yesu Kristu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zetu, na dhambi za dunia nzima.

Kila penye punje ndogo (badala ya Salamu Maria):

MWANZISHAJI: Kwa ajili ya mateso makali ya Bwana wetu Yesu Kristu,

WOTE HUITIKIA: Utuhurumie sisi na dunia nzima.

Mwisho wa Rozari sali sala ifuatayo mara tatu:

Mungu Mtakatifu, Mtakatifu mwenye Enzi, Mtakatifu unayeishi milele, Utuhurumie sisi na dunia nzima.

LITANIA YA HURUMA YA MUNGU.

Bwana utuhurumie –

Bwana utuhurumie

Kristo utuhurumie – Kristo

utuhurumie

Bwana utuhurumie –

Bwana utuhurumie

Kristo utusikie – Kristo

utusikilize

Baba wa mbinguni Mungu –

utuhurumie

Mwana Mkombozi wa dunia

Mungu – utuhurumie

Roho Mtakatifu Mungu –

utuhurumie

Utatu Mtakatifu Mungu mmoja –

utuhurumie.

Huruma ya Mungu iliyo sifa kuu

ya Muumba wetu – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu iliyo kilele cha

ukamilifu wa Mwokozi wetu – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu iliyo upendo

usiopimika wa Roho Mtakasa – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu fumbo

lisilofahamika la Utatu Mtakatifu – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu iliyo ishara ya

uwezo mkuu wa Mungu

Mwenyezi – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu

iliyofumbuliwa katika kuziumba

Roho za Malaika wa mbinguni – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu iliyotuumba

na kutuamuru tuwepo bila

kutokana na chochote – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu inayotujalia

maisha ya kutokufa – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu inayotukinga

na adhabu tunazostahili – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu inayotuinua

tutoke katika taabu, unyonge na

maumivu ya dhambi zetu – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu inayotufanya

wenye haki katika Neno

aliyejifanya Mtu – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu inayofurika

kutoka katika majeraha ya Kristo – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu inayobubujika

kutoka ndani ya Moyo Mtakatifu

wa Yesu – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu iliyotupatia

Bikira Maria Mtukufu awe kwetu

Mama wa Huruma – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu iliyoonyeshwa

katika kuanzishwa Kanisa

Katoliki – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu inayopatikana

katika mafumbo ya Sakramenti

Takatifu – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu inayotolewa

kwa wanadamu wote kwa njia ya

Sakramenti ya Ubatizo na Kitubio – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu inayotolewa

katika Sakramenti ya Ekaristi na

Upadrisho – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu

inayooneshwa kwetu pale

inapotuita na kutuingiza katika

kuwatakatifuza wenye haki – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu inayotimilika

katika ukamilifu wa watu

watakatifu – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu chemchemi ya

afya kwa wagonjwa na wote

wanaoteseka – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu iliyo faraja ya

wote wenye uchungu moyoni – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu iliyo tumaini

la roho zinazosumbuliwa na

mkato wa tamaa – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu iliyo mwenzi

wa daima na popote wa watu

wote – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu inayowahi

kutuletea neema zake – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu iliyo amani

yao wanaokufa – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu iliyo

burudisho na faraja yao

marehemu wa toharani – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu iliyo furaha

ya mbinguni kwa watakatifu wote – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu iliyo taji la

watakatifu wote – tunakutumainia.

Huruma ya Mungu chemchemi ya

miujiza isiyokauka – tunakutumainia.

Mwanakondoo wa Mungu

uliyetuonyesha huruma yako kuu

katika kuikomboa dunia kwa

msalaba wako mtakatifu –

utusamehe ee Bwana

Mwanakondoo wa Mungu

unayejitolea kwetu kwa mapendo

na huruma katika kila adhimisho

la Sadaka ya Misa Takatifu –

utusikilize ee Bwana

Mwanakondoo wa Mungu

anayeondoa dhambi za dunia

kwa njia ya huruma yako isiyo

na mwisho – utuhurumie.

KIONGOZI: Bwana utuhurumie –

WOTE: Kristo utuhurumie.

KIONGOZI: Huruma anana za

Bwana zi juu ya kazi zake zote –

WOTE: Huruma za Bwana

nitaziimba milele.

TUOMBE: Ee Mungu uliye na

huruma isiyo na mwisho, na

hazina za wema na upendo wako

hazina mipaka. Tunakusihi

ututazame sisi watu wako huku

duniani na kutuongezea huruma

yako tena na tena, ili itusaidie

tusije tukakata tamaa hata mara

moja, haidhuru tukumbane na

majaribu makubwa kiasi gani,

bali tuweze daima kuzielekea na

kuzishika amri zako, kwa

matumaini na kutimiza mapenzi

yako matakatifu, ambayo ndiyo

huruma yenyewe. Tunaomba

hayo kwa njia ya Bwana wetu

Yesu Kristu Mwanao, Mfalme wa

Amani na Huruma, aishiye na

kutawala nawe, na Roho

Mtakatifu, kwa pamoja

mkituonyesha huruma, daima na milele.

Amina

Leave a Comment