Mapenzi & Mahusiano

Dalili za Mwanamke mwenye hamu ya tendo la ndoa

Dalili za Mwanamke mwenye hamu ya tendo la ndoa

  1. Kama anazungumzia kuhusu kujamiiana uwapo naye

Kama anaongea kwa kujiamini na ana uhuru wa kutaja mambo mbalimbali yanayohusu kujamiiana kama mkao anaofurahia zaidi wakati wa kujamiiana, vifaa vya vinavyotumika kujiridhisha kingono pamoja na mambo mengine ya kujiridhisha wakati wa kujamiiana, tambua kwamba anataka uendeleze mada hiyo mpaka mjikute mkijamiiana.

Akiamua kuizungumzia kwenye maongezi yenu, yawezekana akawa anakupa ishara kwamba yupo tayari kwa tendo hilo – kilichobaki ni kuomba.

  1. Kama ghafla anavaa nguo zinazoacha maungo yake wazi

Njia rahisi ya kumshawishi mwanaume kujamiiana ni pale mwanamke anapovaa nguo za kichokozi, zinazoacha baadhi ya maumbile yake wazi. Kama umezoea kumuona akiwa anavaa nguo rasmi na ghafla akavaa nguo zinazoacha baadhi ya maumbile yake wazi mkiwa kwenye mtoko au miadi yoyote, basi jiongeze – sio lazima akwambie kwakuwa wanawake wengi hawawezi kumwambia mwanaume kuwa anataka wafanye mapenzi.

  1. Kama anakualika nyumbani kwake

Baadhi ya wanawake wanapojisikia kufanya mapenzi wanaweza kukualika nyumbani kwake ili mfanye anachokitaka bila kulazimika kukwambia lolote.

Atatandika kitanda, kukupikia chakula unachokipenda au kukupa kinywaji chenye pombe ili ulewe kidogo na kisha muendelee kutokea hapo.

  1. Kama anavutiwa na mambo mengi kutoka kwako

Kama anaonesha kuvutiwa zaidi kuliko ulivyozoea siku zote, unatakiwa kujua kwamba yupo tayari kufanya mapenzi na wewe kwa siku hiyo.

Yawezekana akionesha kuvutiwa na wewe kwa kukulegezea sauti au anavyotembea mkiwa mmebaki wawili. Joto la mwili wake linapoongezeka au macho yanapomlegea zaidi. Hii haimaanishi kwamba unatakiwa kumchunguza, ila jaribu kuzingatia kwa makini mabadiliko yanayotokea kuanzia mazungumzo mpaka mwili.

  1. Kama anakugusa sehemu zinazokusisimua

Mwanamke anaweza kuamua kukuonesha kuwa yupo tayari kufanya mapenzi na wewe kwa kushika sehemu za mwili wako ambazo zinakusisimua kama masikio, shingo, mapaja, kifua au miguuni.

1 Comment

Leave a Comment